ESCROW NDIYO HABARI YA MJINI

WAKATI sakata la kuchukuliwa kwa mabilioni ya shilingi katika akaunti ya Tegeta Escrow likiendelea kuwa gumzo la sasa la mjini, sura mpya imeanza kujitokeza kwa watu zaidi wanaohusishwa na kugawiwa salio kutajwa, licha ya waliotajwa awali kuendelea kubakia katika orodha.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Kashfa hiyo iliibuliwa kwa mara ya kwanza na mbunge wa Kigoma Kusini kupitia Chama cha NCCR-Mageuzi, David Kafulila katika kikao cha Bunge lililopita, kitu ambacho kilipingwa kwa nguvu kubwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema pamoja na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.
Hata hivyo, kadiri siku zinavyokwenda hali imeonekana kuwa ni ngumu kwa vigogo wa serikali kwani wanaonekana kama wameshikwa pabaya na wengi wametajwa kuhusika kwa njia moja au nyingine.
Ukiacha Werema, Muhongo na Eliakim Maswi kutajwa kunufaika na uchotwaji wa fedha hizo zilizokuwa Benki Kuu, wengine wanaodaiwa kupata mgao huo ni pamoja na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka, mwanasheria mkuu wa zamani wa serikali, Andrew Chenge na Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania, Profesa Benno Ndullu.
4Aidha vigogo wengine wengi, wakiongozwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, nao wanatajwa kuhusishwa na ukwapuaji wa fedha hizo kutokana na nyadhifa zao.
Lakini wakati Bunge hilo likianza vikao vyake vya wiki hii, Spika wa Bunge, Anne Makinda, naye alitajwa bungeni na Mbunge wa Mkanyageni kwa tiketi ya CUF, Habib Mnyaa kuwa anadaiwa kupewa mgao wa dola milioni moja za Marekani.
Kana kwamba haitoshi, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali, katika kijarida maalum kilichochapishwa kumchafua kilichosambazwa Dodoma, naye anatajwa kuchukua mlungula kutoka kampuni inayohusishwa na sakata hilo ya PAP.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka.
Akaunti ya Tegeta Escrow ilifunguliwa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) ili kutunza fedha ambazo Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) zilipaswa kuilipa kampuni ya kufua umeme wa IPTL kwa kuiuzia nishati hiyo.
Hiyo ilitokana na shirika hilo la umma, kushtaki katika mahakama ya kibiashara ikilalamikia bei kubwa iliyotozwa na IPTL na kusababisha kufunguliwa kwa akaunti hiyo ili fedha hizo ziwekwe huko hadi muafaka baina ya pande hizo mbili utakapopatikana.
Hata hivyo, kabla ya muafaka huo kupatikana, wajanja walikwenda na kuzichukua fedha hizo ambazo sasa zinawatokea puani
ESCROW NDIYO HABARI YA MJINI ESCROW NDIYO HABARI YA MJINI Reviewed by Unknown on 9:24:00 PM Rating: 5
Powered by Blogger.