MSANII wa
Bongo Fleva zao la nyumba ya kukuza vipaji Tanzania ‘THT’, Amini
Mwinyimkuu jana jioni alifanyiwa hafla fupi ya kuagwa na uongozi wa THT.
Tukio hilo lilifanyika ndani ya ofisi
hizo zilizopo Kinondoni jijini Dar es Salaam, karibu kabisa na Viwanja
vya Leaders Club ambapo Amini alipata muda wa kuwaaga baadhi ya wasanii
wenzake na uongozi kwa ujumla wa THT.
Akizungumza kwenye hafla hiyo alisema
kwamba ameamua kuondoka mikononi mwa chuo hicho baada ya kupata kampuni
mpya ya BME CO LTD,ambayo itasimamia kazi zake zote za muziki ingawa
atabaki kushiriki kwenye kazi maalum za THT pindi atakapohitajika.
Kupitia hafla hiyo, Amini aliweza kutoa
vyeti na tuzo za shukurani kwa baadhi ya viongozi wake wa juu na walimu
wote waliomsaidia kukuza kipaji chake wakati akiingia kwenye chuo hicho
cha muziki.
AMINI AJIONDOA THT, AAGWA KWA NDEREMO
Reviewed by Unknown
on
7:43:00 AM
Rating: