Sakata la mke kuishi na waume wawili  
limechukua sura mpya baada ya kikao cha ndugu wa mume halali, Rogers 
Halinga kuketi kikao katika Kijiji cha Ishungu, Kata ya Ruiwa Mbarali, 
mkoani Mbeya na kumtaka Biton Mwashilindi kufanya mazungumzo nao kabla 
hawajafungua madai ya ugoni mahakamani na kudai fidia.
Kikao hicho kizito kilichofanyika 
nyumbani kwa baba mzazi wa Rogers, mzee Jason Halinga (95), Novemba mosi
 mwaka huu na kuhudhuriwa na ndugu lukuki nia ilikuwa kumsikiza mke wa 
Rogers, Juliana (22)  ili abainishe ukweli juu ya mtoto aliyezua utata 
kuwa ni wa nani baina ya mumewe (Rogers) na Biton Mwashilindi.
Mwanamke huyo  akijikanganya mara kadhaa
 katika kikao hicho akidai mtoto huyo ni wa Rogers, kwani aliondoka 
baada ya kutokea mabishano na mumewe akiwa na ujauzito wa miezi minne 
ndipo alipoanza mahusiano ya kimapenzi na Biton hadi siku anajifungua 
mwaka 2012 akiwa mikononi mwa Biton na aliamua kumwandikisha mtoto 
katika kadi ya kliniki kuwa baba yake ni Biton.
Kutokana na kauli hiyo, ndugu wa Rogers 
walikuja juu na kumtaka Juliana atamke wazi mtoto ni wa nani ndipo 
alijibu kuwa mtoto ni wa Biton Mwashilindi, ambapo alimkabidhi mtoto 
huyo mwishoni mwa Oktoba kwa hiari yake na wala hakuporwa kama alivyotoa
 taarifa polisi.
Kauli hiyo ya Juliana iliwafanya ndugu 
wa mume kupiga simu kwa mzazi wa Juliana anayeishi Lwanjilo wilayani 
Chunya kujua mustakabali wa kauli ya mtoto wao kwani ilidaiwa kuwa Biton
 aliwahi kwenda huko kujitambulisha kuwa yeye anaishi na mtoto wao kwa 
kuwa hakujua kuwa Juliana aliwahi kuolewa kwani alidai kuwa yeye ni 
mwanafunzi wa VETA Mbeya.
Baba mzazi wa Juliana,  Hosea Mwalukasa 
alipopigiwa simu alidai kuwa ni kweli Biton alifika kwake lakini 
hakumpokea kwa kuwa alidai kuwa Juliana ni mke halali wa Rogers Halinga,
 akawaambia kuwa kama amezaa na Juliana amefanya kosa na kwamba atatozwa
 faini ya ugoni kwani mwanaye hakuwahi kupewa talaka na Halinga.
Baada ya mvutano wa muda mrefu kikao 
kiliamua kuwa endapo Biton anadai kuwa mtoto aliyezaliwa na Juliana 
aliyefahamika kwa jina la Zalida Biton (2) ni wake basi alipe fidia ya 
kuzaa na mke wa mtu kiasi cha shilingi milioni kumi au n’gombe saba ili 
aweze kumkomboa mtoto wake na kwamba Juliana bado ni mke halali wa 
Rogers.
Kwa upande wake Biton alidai kuwa hayuko
 tayari kulipa faini hiyo kwa sababu alikabidhiwa mtoto kihalali na 
Jeshi la Polisi Oktoba 31, mwaka huu katika Kituo Kikuu cha Kati  mbele 
ya maafisa wa polisi na kwamba hana kesi ya kujibu na anasubiri mtoto 
afikishe umri wa miaka saba ndipo amchukue.
“Baadhi ya wadau wamelilalamikia Jeshi 
la Polisi Tanzania kwa kuamua  masuala ya kisheria katika vituo vya 
polisi badala ya kufikisha katika mamlaka za kisheria kama mahakama. 
Uamuzi uliotolewa umesababisha tatizo kuwa zito,” alisema ndugu wa 
Rogers aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini.
Amedai kitendo cha kukabidhiwa mtoto Biton bila kuchukuliwa kipimo cha DNA bado hakijatatua mgogoro huo na kwamba suluhu katika ndoa hiyo ni kitendawili kisicho na majibu.
Amedai kitendo cha kukabidhiwa mtoto Biton bila kuchukuliwa kipimo cha DNA bado hakijatatua mgogoro huo na kwamba suluhu katika ndoa hiyo ni kitendawili kisicho na majibu.
CHUNGU YA NDOA..!! MKE ANAYEISHI NA WAUME WAWILI MAPYA YAIBUKA 
 
        Reviewed by Unknown
        on 
        
10:50:00 PM
 
        Rating: