Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kimefikia Tamati yake

Maoni Kutoka Kwa Mdau
Si kificho tena, bali ni uhalisia, Chama cha Demokrasia na Maendeleo, kimefikia tamati yake kabla hata ya uchaguzi mkuu wa oktoba kufikia.

Ni jambo ambalo wenyewe wanaweza lipinga lakini viashiria vyote vya chama hai havionekani kwa Chadema.

Hakuna uibuzi wa hoja zenye kuleta suluhisho la changamoto tulizonazo kama taifa, bali tunasikia tu mipasho kila kona ya nchi hii toka kwa viongozi wake.

Safu ya juu ya chama imekosa ubunifu na kubaki kulaumu kila mtu mpaka wale wasiohusika.

Si kificho tena bali ni uhalisia, Chadema imeishia njiani, kutokana na ulafi wa madaraka na ubinafsi.

Chadema kinapumulia mwavuli wa UKAWA na hoja ya katiba mpya , bila hiyo hawana la kutuambia watanzania.

By Stroke/JF
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kimefikia Tamati yake Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Kimefikia Tamati yake Reviewed by Unknown on 2:51:00 PM Rating: 5
Powered by Blogger.