ZARI MPENZI MPYA WA DIAMOND PLATNUM ATUA NDANI YA DAR KWA MARA YA KWANZA==>>ATHIBITISHA KUWA YEYE NI MPENZI WA DIAMOND



Katika mitoko yako ya weekend hii usije kushtuka utakapokutana na couple fulani ‘Ameizing’ ya TZ+UG, sababu Zari Tlale a.k.a The Boss Lady yupo ndani ya jiji la Dar au kama anavyopaita mrembo huyo D-City.


Kupitia Instagram mrembo huyo....



wa Uganda ambaye makazi yake yako Afrika Kusini amepost picha kadhaa akiwa na mpenzi wake Diamond Platnumz kwenye gari ya staa huyo aina ya BMW.

Katika picha nyingine inayothibitisha uwepo wake ndani ya jiji la joto, ni picha aliyopiga na mpenzi wa dancer wa Diamond, dumyutamu anayejiita jujudumyz.

Kwenye moja ya picha hizo ameandika : “Another beautiful day in D-City”, na kwenye picha nyingine ameandika moja ya misemo inayovuma kwa sasa hapa mjini“Kishkwambiii”.

Licha ya kwamba Diamond na Zari kwa sasa wanajulikana kuwa ni wapenzi, lakini mara zote walipoulizwa juu ya uhusiano wao wamekuwa wakikanusha na kusisitiza kuwa wana project ya pamoja. Lakini safari hii Zari amethibitisha mwenye kwa kauli yake baada ya kumuita girlfriend wa dancer wa Diamond “wifi”.


Kwenye picha aliyopiga na msichana huyo Zari ameandika: “With wifi @jujudumyz out and about D-City”

Hivi karibuni Diamond alithibitisha kuwa anategemea kupata mtoto na Zari baada ya kupost picha ya Ultra Sound ikithibitisha kuwa Zari ni mjamzito. Hivyo huenda Diamond atakuwa anafurahia kukishika kitumbo kinachokua cha Zari ambamo ndani yupo Chibu Junior.
ZARI MPENZI MPYA WA DIAMOND PLATNUM ATUA NDANI YA DAR KWA MARA YA KWANZA==>>ATHIBITISHA KUWA YEYE NI MPENZI WA DIAMOND ZARI MPENZI MPYA WA DIAMOND PLATNUM ATUA NDANI YA DAR KWA MARA YA KWANZA==>>ATHIBITISHA KUWA YEYE NI MPENZI WA DIAMOND Reviewed by Unknown on 11:25:00 AM Rating: 5
Powered by Blogger.