Wema Sepetu Kortini Kwa Uwizi wa Umeme..Tanesco Waeleza Makubwa

KIMENUKA! Baada ya Miss Tanzania 2006 aliye pia nyota wa sinema za Bongo, Wema Sepetu ‘Madam’ kunaswa na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) akidaiwa kutumia umeme wa shirika hilo kinyemela, kuna madai atapandishwa kortini.
Taarifa kutoka chanzo makini zinasema kuwa, mrembo huyo alifanya ‘manuva’ hayo katika nyumba anayoishi, Kijitonyama, Dar hivyo kuweza kuliingizia hasara shirika hilo hali ambayo shirika hilo haliwezi kumvumilia.


“Amefanya ile michezo ya kuchezea mita. Mita inakuwa inasoma umeme mdogo lakini mzigo unaotumika ndani mkubwa, haufanani na malipo halisi ambayo alistahili kulipia,” kilisema chanzo chetu na kuongeza:
“Maofisa wa Tanesco juzikati ndiyo wakampitia. Inasemekana Wema alikuwa ndani na Idris (yule mshindi wa Big Brother Africa). Idris ndiye alitoka lakini Madam hakuinua miguu yake kwenda nje, wakamng’olea mita na kuondoka nayo.”

Baada ya chanzo hicho kuvujisha ubuyu huo sambamba na picha zilizosemekana ni za siku ya tukio wakati maofisa hao walipofika nyumbani hapo na kufanya ‘ambushi’, paparazi wetu alimpigia simu Wema kwa muda mrefu lakini hakupatikana, akampigia mtu wa karibu na Madam, Ahmed Hasheem ‘Petit Man’ ambapo alipatikana na kusema:

“Unajua kaka mimi si msemaji wa Wema. Mimi ni msemaji wa wasanii walio kwenye lebo ya Wema ya Endless Fame. Kama unataka msemaji wake, cheki na Martin Kadinda.”
Alipotafutwa Martin, alijibu kwa kifupi: “Kaka hata mimi nazisikia hizo habari lakini sipo Dar, nikirudi nitakwenda kucheki halafu nitakupa taarifa kamili.”
Juzi Jumanne, paparazi wetu alifika nyumbani kwa Wema ili kujionea sakata hilo lakini hakufanikiwa kuingia getini baada ya kugonga geti kwa muda mrefu bila majibu.
Mmoja wa majirani wa mrembo huyo aliyeomba hifadhi ya jina, alipoulizwa kuhusu kufahamu sakata hilo, alisema:

“Kiukweli sisi wenyewe tulishangaa. Tunaamini Madam si mtu kuchezea mita. Ni mtu anayejiweza, anayejitambua sasa tumeshtuka kuona mita inatolewa.”
Paparazi wetu alifika Ofisi za Tanesco Mkoa wa Kinondoni Kaskazini (Mikocheni) ili kuzungumza na wahusika lakini akakosa ushirikiano.

Hata hivyo, mfanyakazi mmoja wa Kitengo cha Emergency (Dharura) aliyeomba kufichwa jina lake, alisema ni kweli zoezi hilo lilifanyika nyumbani kwa Wema, Jumatatu iliyopita na kukutana na kadhia hiyo ambapo alisema madam huyo atapandishwa mahakamani kujibu mashitaka ya kuiibia Tanesco.
GPL
Wema Sepetu Kortini Kwa Uwizi wa Umeme..Tanesco Waeleza Makubwa Wema Sepetu Kortini Kwa Uwizi wa Umeme..Tanesco Waeleza Makubwa Reviewed by Unknown on 10:21:00 AM Rating: 5
Powered by Blogger.